January 25, 2014

EYMAEL

Pamoja na kukosa nafasi ya kuinoa Yanga aliyokuwa akiitaka kwa udi na uvumba, imeelezwa Luc Eymael anaweza kupata nafasi ya kuinoa timu ya taifa ya Rwanda.


Eymael raia wa Ubelgiji alikuwa kati ya makocha wanaowaniwa kuinoa Yanga ambayo mwisho ilimnasa, Hans van Der Pluijm.

Mmoja wa rafiki wa karibu wameiambia SALEHJEMBE, Eymael amekuwa kwenye mazungumzo wa na viongozi wa Shirikisho la Soka la Rwanda (Ferwafa).

“Sijajua vizuri kama wanataka akafundishe timu ya taifa au wanazungumza naye kwa niaba ya klabu fulani.
“Lakini najua watu wa Rwanda wanamhitaji Eymael, tusubiri ndani ya siku mbili hizi tutajua,” alisema rafiki yake huyo.

Eymael amewahi kuinoa AFC Leopards ya Kenya na wakati anawaniwa na Yanga alikuwa kwao Ubelgiji.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic