January 25, 2014



Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amesema ushindi kwa Rhino Rangers ya Tabora utakuwa bora kuliko wote watakaopata kwenye Ligi Kuu Bara.


Logarusic raia wa Croatia amesema, kama wataishinda Rhino, watakuwa na uhakika wa kujenga upya hali ya kujiamini na kushinda mechi nyingine.

“Tunauhitaji ushindi wa Jumapili kupita mwingine wowote, huo ndiyo utakaotupa dira tunakwenda wapi na nini cha kufanya.
“Kama tutashinda maana yake tunaweza kujenga hali ya kujiamini na kujua cha kufanya.

“Wachezaji wanalijua hilo, ninawaamini watafanya kila kitu kwa uhakika na kushinda mechi,” alisema Logarusic.

Simba inaanza kampeni za lala salama ya Ligi Kuu Bara, kesho kwa kuivaa Rhino ya Tabora ambayo walitoka nayo sare ya mabao 2-2 katika mzunguko wa kwanza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic