January 25, 2014

TALIB HILAL (KUSHOTO) AKIKABIDHI VIFAA KWA MWENYEKITI WA COASTAL UNION, AURORA. KATIKATI NI OFISA WA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI OMAN.
Kocha wa timu ya taifa ya vijana ya ufukweni ya Oman, Talib Hilal amesema kuwajali vijana ndiyo nguzo ya soka bora.


Akizungumza kutoka Oman, Hilal aliyewahi kukipiga Simba, amesema mipango ya kuendeleza soka inaanza kwa vijana na lazima kila timu ilitilie mkazo suala hilo.
“Mkiwa na msingi mzuri kwa vijana, lazima mnakuwa na uhakika wa maendeleo katika soka.

“Hivyo lazima kuwapa nafasi vijana, wafundishwe na walimu bora, watumie vifaa bora na wawekewe mazingira mazuri.
“Kama ni vipaji, Tanzania ina vipaji vingi sana na vinaweza kufanya vizuri kama utaratibu utafuatwa,” alisema Talib.

Hivi karibuni, Talib alimwaga vifaa kwa timu ya vijana ya Coastal Union ambayo ilishinda michuano ya Uhai Cup.

Hiyo ilikuwa ni mara ya pili kutoa msaada kwa timu ya vijana baada ya kutoa vifaa kwa ile ya Simba, hata hivyo inaelezwa, havikufika.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic