January 29, 2014


Maafande wa Ruvu Shooting wameshindwa kuvunja rekodi ya Mbeya City ambayo haijafungwa hata mechi moja tokea kuanza kwa Ligi Kuu Bara.


Katika mechi ya ligi hiyo leo kwenye Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi, Pwani, timu hizo zimetoka sare ya bao 1-1.
Wenyeji ndiyo walianza kupata bao, lakini Mbeya City wajaonyesha ni wabishi na kufanikiwa kusawazisha na ndiyo yakawa matokeo hadi mwisho.

Awali Ruvu kupitia msemaji wao, Masau Bwire walisema wangeivunja rekodi hiyo ya Mbeya City ambayo imekuwa ikipata matokeo ya sare na ushindi tu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic