January 6, 2014

CHEKA AKIMTWANGA MMAREKANI NA KUTWAA MKANDA JIJINI DAR

Bondia Francis Cheka amefunguka kuwa, njaa ndiyo iliyosababisha apokonywe mkanda wake wa WBF kwa kuwa alikuwa hana jinsi ndiyo maana alikwenda kupigana nje ya nchi.


Cheka alipokonywa mkanda wake wa WBF kwa kupigwa kwa KO na Mrusi, Fedor Chudinor alipokwenda kucheza kwenye Ukumbi wa Dynamo Palace of Sports, Krylatskoye, Urusi, Desemba, mwaka jana.
 
CHEKA NA SALEH ALLY
Cheka alisema njaa ndiyo iliyomfanya aende kupigana nchini humo kwa kuwa hakuwa na fedha, kwani hata yeye mwenyewe aliona hana uwezo wa kumpiga bondia huyo kutokana na maandalizi hafifu aliyoyafanya.

“Sikuwa na maandalizi mazuri, nilikosa fedha, hali iliyosababisha niuze mifuko yangu ya simenti na matofali ndiyo nifanikiwe kwenda kupigana. Kwa kifupi njaa ndiyo iliyonipeleka kule, sikuwa na maandalizi,” alisema Cheka.

Bondia huyo ndiye bora zaidi kwa kipindi hiki lakini amekuwa akilalamika malipo kidogo anayoyapata kutoka kwa mapromota yanapunguza kasi ya maendeleo yake.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic