January 6, 2014



Aliyekuwa Kocha Msaidizi wa Yanga, Fred Felix Minziro, amesema yupo tayari kurudi kuifundisha timu hiyo muda wowote endapo uongozi wa klabu hiyo utahitaji huduma yake, licha ya kumtimua hivi karibuni.


Uongozi wa Yanga uliwatimua Minziro pamoja na makocha wenzake, Ernie Brandts aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo na Razack Siwa aliyekuwa kocha msaidizi, kutokana na kutoridhishwa na utendaji wao wa kazi.

Minziro amesema licha ya kutimuliwa na Yanga, bado ana mapenzi ya dhati na timu hiyo na endapo uongozi utahitaji huduma yake, basi atarejea kuendelea na kazi yake hiyo.

Alisema hana kinyongo na viongozi wa timu hiyo, licha ya maamuzi makali waliyoyachukua dhidi yake na kwamba ameyapokea kwa mikono miwili.

"Hivi sasa nahitaji kupumzika kwanza kwa sababu timu zote za ligi kuu zina makocha wao, labda nitaanza harakati za kutafuta kazi mwishoni mwa msimu huu.

"Hata hivyo kama uongozi wa Yanga utahitaji huduma yangu kwa mara nyingine, basi mimi nipo tayari kurudi kwa sababu nina mapenzi ya dhati na klabu hiyo," alisema Minziro.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic