January 27, 2014


Nahodha na beki wa pembeni wa Simba, Said Nassor ‘Chollo’, amelazimika kupumzishwa kwenye timu hiyo kwa ajili ya kupisha matibabu anayofanyiwa kwa sasa.

Chollo aliyekumbwa na majeraha mfululizo ndani ya kipindi kifupi, ameanza matibabu mara baada ya vipimo vilivyofanyika Ijumaa katika hospitali inayofahamika kwa jina la Doctors Plaza iliyopo Upanga, Dar kuonyesha kuwa ana tatizo kwenye nyonga yake ya kushoto.

 Ofisa Habari wa Simba, Asha Muhaji, alisema matibabu hayo yatachukua wiki tatu.
Alisema kuwa beki huyo atakapomaliza matibabu hayo, atahitajika kuchukuliwa tena vipimo vya kina kwa ajili ya kujiridhisha kama tatizo hilo litakuwa limekwisha au la.
“Kwa sasa Chollo atakaa nje ya uwanja kwa muda wa wiki tatu akiendelea na matibabu huku akihitajika kuhudhuria hospitalini mara kwa mara ndani ya muda huo ambapo kwa mujibu wa madaktari waliomtibu, muda huo ukimalizika, atafanyiwa tena vipimo kuangalia tatizo kama litakuwa limekwisha,” alisema Muhaji.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic