January 27, 2014


Sakata la mshambuliaji wa Yanga SC, Emmanuel Okwi kuzuiwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuichezea klabu hiyo, limeifanya Yanga kuweka kando kwa sasa suala la kiungo wake Athumani Idd ‘Chuji’.


Okwi alisimamishwa na shirikisho hilo siku mbili kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi kwa madai ya kutaka kujiridhisha na usajili wa raia huyo wa Uganda kutoka Klabu ya Villa ya Uganda huku akiwa na mgogoro na Etoile du Sahel ya Tunisia.

Yanga sasa imekuwa ‘bize’ kuhakikisha inalitatua suala hilo mapema haraka iwezekanavyo huku majadiliano juu ya msamaha wa Chuji yakiendelea kusubiri pembeni.

Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu, alisema bado hajajua kinachoendelea kuhusu Chuji kwa kuwa kuna vitu vingi vilijitokeza hapa kati na vinahitaji kuwekwa sawa haraka iwezekanavyo, likiwemo suala la Okwi.

Alisema sakata la Okwi ambaye ni mchezaji wa zamani wa Simba, lilikuja ghafla mezani kwake hivyo kutokana na majukumu hayo, mpaka sasa hajapokea taarifa ya kinachoendelea kwa Chuji kutokana na kuwa na kazi hiyo nyingine inayohitaji utatuzi wa haraka.
Alifafanua kuwa, kuna kamati maalum inayolishughulikia sakata la kiungo huyo ambayo mpaka sasa bado haijampa taarifa ya kinachoendelea juu ya hayo yote ambapo inaonekana dhahiri kuwa likimalizika la Okwi ndiyo la Chuji litajadiliwa.

 “Hapa kati kulikuwa na muingiliano wa vitu vingi vilivyohitaji kushughulikiwa kwa haraka zaidi, kulikuwa na maandalizi ya ligi, suala la Okwi kwa hiyo mezani kwangu hayo yakawa yamechukua hatamu kwa kuwa yalihitaji uharaka zaidi.

“Ila kuhusu suala la Chuji bado lipo ingawa kuna kamati inayolishughulikia hili ambayo bado haijanijuza nini kinaendelea na sijajua kama inaweza kukaa tena lini kujadiliana lakini kwa sasa kubwa nililonalo ni hili la Okwi,” alisema Njovu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic