January 10, 2014





Kiungo aliyesimamishwa kwa muda usiojulikana na klabu yake ya Yanga, Athumani Idd ‘Chuji’, jana asubuhi alikabidhi barua ya kuomba radhi kwa uongozi wa klabu hiyo iliyopo Mtaa wa Jangwani.
 
Moja wa viongozi wa klabu hiyo ambaye aliomba jina lake lihifadhiwie kutokana na yeye kuwa si msemaji wa klabu hiyo alisema kuwa majira ya saa tano asubuhi Chuji alifika klabuni na kukabidhi barua hiyo ambayo inamaelezo ndani yake ya kuomba radhi.

“Chuji alikuja asubuhi akaonana na baadhi ya viongozi wa klabu na kukabidhi barua hiyo lakini kuhusu kumsamehe au kutomsamehe jukumu lote ameachiwa (Abdallah) Bin Kleb,” alisema kiongozi huyo.

Chuji hakupokea simu yake wakati Bin Kleb hakupatikana kulizungumzia hilo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic