January 10, 2014




Makipa wa Yanga wamevimba nyonga ‘hips’ kutokana na mazoezi makali ambayo wamekuwa wakipewa na kocha wao wa makipa, Juma Pondamali.


Makipa hao ni Juma Kaseja, Ally Mustafa ‘Barthez’, Deogratius Munishi ‘Dida’ na Yusuf Abdul.

SALEHJEMBE ilishuhudia makipa wote wakilalamika kuvimba nyonga kutokana na mazoezi ya Pondamali.

Alipoulizwa Pondamali juu ya hilo, alisema: “Makipa wangu wanalalamika sana wamevimba hips kutokana na mazoezi ninayowapa, ni kweli lakini wajue hapo nawaongezea uwezo zaidi na nitaongeza,” alisema Pondamali.

Wakati huohuo, kabla ya kuondoka, Yanga ilikuwa ikifanya mazoezi kwenye Viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe jijini Dar ambapo pembeni kidogo na walipokuwa wakifanya mazoezi kulikuwa na kinyesi cha ng’ombe.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic