January 22, 2014





Timu ya Coastal Union inatarajiwa kurejea nchini kesho, huku ikiahidi kufanya mambo makubwa kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara mzunguko wa pili.


Coastal ipo nchini Oman kwa wiki mbili kwa ajili ya kujiandaa na mzunguko huo wa pili wa ligi kuu, ikiwa chini ya kocha wao mpya, Yusuph Chippo.
 
Mwenyekiti wa timu hiyo, Mohamed Aurora, alisema timu hiyo inarejea ikiwa na matumaini ya kuanza vyema katika ligi kutokana na maandalizi waliyofanya huko.
 
Aurora alisema wamejifunza mengi walipokuwa huko na wamecheza mechi za kirafiki na timu za ligi kuu na moja ya Ligi Daraja la Pili ambazo zimeweza kuwajenga kwa kiasi kikubwa na kuwa imara zaidi.
“Timu itarejea nchini ikiwa na matumaini ya  kufanya vyema kutokana na maandalizi tuliyoweza kufanya huku.  Ilifika kipindi tulibadili muda wa mazoezi  ili kuendana na hali ya hewa ya kwetu.
“Lakini kikubwa tunashukuru mipango na malengo yetu yamekwenda vizuri na ninaamini katika mzunguko huu wa pili, Coastal itakuwa nyingine kutokana na mabadiliko  ambayo yametokana na maandalizi tuliyofanya huko ili kuweza kuwa katika nafasi nzuri,” alisema Aurora.

Coastal ilimaliza mzunguko wa kwanza ikiwa katika nafasi ya nane na pointi 16.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic