January 22, 2014





Kocha Mkuu wa Ashanti United, Abdallah Kibadeni, amesema atahakikisha anaifunga Yanga kwenye mechi ya kwanza ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara mzuguko wa pili Jumamosi.
 
Yanga ipo Uturuki kwa takribani wiki mbili sasa kwa ajili ya maandalizi ya mzunguko wa pili wa ligi na michuano ya Klabu Bingwa Afrika ambapo inatarajia kurejea nchini kesho Alhamisi, lakini Kibadeni, kocha wa zamani wa Simba, amesema hata iweje watawazima tu.

Kibadeni alisema kuwa hawezi kuihofia Yanga kwa kuwa imeenda kujiandaa Uturuki ambapo anaamini kuwa maandalizi ni mahali popote pale na wala hawawezi kufungwa kirahisi kwa kuwa wao Ashanti waliweka kambi Bamba Beach, Kigamboni, Dar es Salaam.

“Nia yetu ni kuibuka na ushindi na wala si kingine, japokuwa inategemea mtu utacheza vipi siku hiyo, lakini hatutakuwa na hofu kwamba tunacheza na Yanga ya Uturuki, hatuwezi kuhofia hilo, maandalizi ni popote tu, wao wapo Uturuki sisi tupo Bamba, lakini mechi ndiyo itaamua nani alijiandaa vizuri,” alisema Kibadeni.

Kwenye mechi ya mzunguko wa kwanza wa ligi, Yanga iliyokuwa chini ya Mholanzi, Ernie Brandts, iliifumua Ashanti iliyokuwa chini ya Hassan Banyai mabao 5-1. 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic