January 20, 2014


Kiungo Hassan Dilunga amepata nafuu baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa malaria akiwa nchini Uturuki.

Dilunga yuko na Yanga nchini humo katika kambi ya wiki mbili kujiandaa na Ligi Kuu Bara na Ligi ya Mabingwa Afrika.

Msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto amesema Dilunga yuko katika hali nzuri ukilinganisha na jana na juzi.

“Sasa anaendelea vizuri kabisa, naweza kusema amepona ukilinganisha na siku mbili zilizopita,” alisema Kizuguto.

Aidha, Kizuguto pia alikamatwa na malaria, hata hivyo ameeleza kumaliza dozi na hali yake ni nzuri pia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic