January 5, 2014


Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts ameushukuru uongozi wa Yanga na wadau wote waliomuunga mkono.


Brandts, beki wa zamani wa Roda JC na timu ya taifa ya Uholanzi amesema anaushukuru uongozi huo wa Jangwani pamoja na wadau wote wa soka, lakini pia mashabiki wa Yanga.

“Nafikiri nitaondoka ndani ya siku mbili kurejea nyumbani, muda wangu hapa umeisha. Acha niende, lakini nawashukuru sana.

“Uongozi hata kama kulikuwa na kasoro, lakini wadau mbalimbali na mashabiki wa Yanga ambao walikuwa muhimu sana.
“Waambie wachezaji nawatakia kila la kheri na kuna wale waliokuwa na matatizo, basi warekebishe ili kuendelea kuisaidia Yanga,” alisema.

Brandts aliingoza Yanga kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita.
Wakati uongozi unamfukuza kikosi chake ndiyo kinachoongoza ligi hadi mzunguko wa kwanza ulipofikia mwisho.

Yanga ilimfukuza baada ya kufungwa kwa mabao 3-1 dhidi ya Simba katika mechi ya kirafiki ya Nani Mtani Jembe.

Hata hivyo wadau wamekuwa wakilalamika kwamba si sahihi kwa kuwa kocha kama yeye hapaswi kufukuzwa kwa mechi ya kirafiki.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic