January 5, 2014



Simba imemaliza siku vizuri leo kwa kufanikiwa kufuzu kucheza robo fainali ya michuano ya Mapinduzi.


Simba imefuzu baada ya kuwachapa KMKM ya Zanzibar kwa bao 1-0 lililofungwa na mkongwe Amri Kiemba maarufu kama Baba Shabani.
Bao hilo lilifungwa katika dakika ya 6 baada ya Kiemba kuruka na kuunganisha kwa kichwa krosi krosi safi ya Ali Badru.

Kwa mara ya kwanza Kocha Mkuu, Zdravko Logarusic alikuwa amerejea kwenye benchi la timu hiyo.
Awali Simba iliongozwa mechi mbili za mwanzo na kocha wake msaidizi, Selemani Matola.
Kikosi kamili cha Simba kilipangwa hivi:
Yaw Berko, William Lucian ‘Gallas’, Omar Salum/Miraj Athumani, Gilbert Kaze ‘Demunga’, Donald Mosoti/Joseph Owino, Abdulhalim Humud, Uhuru Selemani/Said Ndemla, Amri Kiemba, Betram Mwombeki/Zahor Pazi, Ali Badru na Edward Chistopher/Adeyum Saleh.


Kikosi cha KMKM; Mudathir Khamis, Pandu Hajji, Haidhurun Juma, Khamis Ali, Iddi Kambi, Ibrahim Khatibu, Nassor Omar/Hajji Simba, Maulid Kapenta, Vincent Kamanya na Machano Abdallah.    

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic