January 6, 2014


Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amesema kikosi chake kutwaa Kombe la Mapinduzi si ishu kubwa sana kwake.


Logarusic ambaye ameungana na Simba akitokea kwao Croatia amesema ataitumia michuano hiyo kama sehemu ya kuboresha kikosi hicho
“Tunacholenga sisi ni Ligi Kuu Bara. Michuano hii ni kama ya kirafiki, tunaweza kuchukua au kutochukua ubingwa na haitakuwa ishu kubwa sana.
“Nataka kutengeneza kikosi changu vizuri zaidi ndiyo maana niliamua kuwa wachezaji ambao hawakupata nafasi katika mechi dhidi ya Yanga, watapata nafasi huku Zanzibar,” alisema Logarusic.
Kocha huyo alisisitiza wachezaji watatakiwa kumuonyesha kwamba wanaweza kila atakapowapa nafasi la sivyo watapoteza kabisa sifa ya kuwa katika kikosi chake.
Jana wakati Simba inaivaa KMKM, Logarusic alisema kipa Yaw Berko na kiungo Abdulhalim Humud ni kati ya watakaopata namba.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic