January 27, 2014


 
PICHA HII, SIKU YANGA WALIPOONDOKA NCHINI KWENDA UTURUKI
Mabingwa wa soka Tanzania, Yanga wameondoka leo alfajiri kwenda Tanga kuivaa Coastal Union.


Yanga imeondoka na kikosi kizima, akiwemo Kocha mpya, Hans van der Pluijm ambaye itakuwa ni mechi yake ya kwanza ugenini baada ya kuingoza Yanga kuifunga Ashanti United bao 2-1.

Meneja wa Yanga, Hafidhi Saleh amesema wameamua kuondoka alfajiri wakiwa na basi lao ili ikiwezekana wafanye mazoezi leo.
Yanga inaivaa Coastal Union keshokutwa Jumatano katika mechi inayosubiriwa kwa hamu.
Coastal Union iliyokuwa imeweka kambi nchini Oman, itakuwa na kazi kubwa ya kujiuliza baada ya kuanza ligi kwa sare ya bao 1-1 ikiwa hapo Mkwakwani.

Wakati Yanga iliyoanza ligi kwa ushindi lakini ikacheza vibaya, italazimika kujituma zaidi kwa kuwa mechi ya timu hizo katika mzunguko wa kwanza ilimalizika kwa sare ya bao 1-1 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic