January 10, 2014





Pamoja na taarifa za awali kueleza beki Shomari Kapombe amerejea Ufaransa kuungana na timu yake ya AS Cannes, taarifa za uhakika zinaeleza bado amekwama nchini na amejichimbia kwao mkoani Morogoro.
 

Kapombe ameendelea kuwepo nchini tangu Desemba, mwaka jana aliporejea kuitumikia timu ya taifa, katika mechi ya kirafiki dhidi ya Zimbabwe, ambapo inaelezwa kutokana na safari yake kutoeleweka, amekuwa hapendi kuonekana hadharani kukwepa maswali.

Mtu wa karibu wa mchezaji huyo ameliambia gazeti hili kuwa, kuna vitu havijakamilika ndiyo maana ameshindwa kuondoka.

Awali, Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) lilihojiwa na gazeti hili na kusema lilimsaidia kukamilisha kila kitu kwa ajili ya safari yake.

“Sasa hivi itakuwa zaidi ya miezi miwili, kuna masuala yake yamemkwamisha, mara nyingi anakuwa kwao Morogoro lakini muda wowote ataondoka,” alisema mtu huyo.

Championi Ijumaa lilimpigia Kapombe simu kupitia namba yake ya Tanzania, ambapo alipokea na kusema: “Nitakupigia baadaye.” Kisha akakata, alipopigiwa baadaye, simu iliita bila kupokelewa.

Alipoulizwa Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura, alisema: “Sisi tulimkamilishia kila kitu, hivyo kama amekwama au la, hilo sisi hatujui.” 
SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic