January 10, 2014





Kukosekana kwa kiungo mzoefu Athumani Idd ‘Chuji’ kwenye msafara wa Yanga uliotua nchini Uturuki kwa ajili ya kambi, kumewasikitisha wachezaji wenzake kadhaa ambao wamesema wanatamani wangekuwa naye.


Beki na nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amesema Chuji ni mchezaji muhimu hasa katika mechi za kimataifa, ndiyo maana kukosekana kwake katika safari kumekuwa ni pigo.

“Naamini pengo la Chuji litazibwa lakini si kwa urahisi hivyo kwa sababu angekuwa msaada mkubwa kwenye mechi za kimataifa, ni mzoefu na mkongwe pia kwenye soka, hivyo vinachangia umuhimu wake kwa kiasi kikubwa,” alisema Cannavaro.

Naye mshambuliaji wa Yanga, Hamis Kiiza, amesema anaamini umuhimu wa Chuji ni mkubwa lakini hawezi kuingilia amri ya uongozi.

“Sina la kusema kwa kuwa uongozi wa timu ndiyo umefanya hilo lakini umuhimu wake uwanjani unajulikana,” alisema Kiiza.

Yanga inatarajia kufungua dimba kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kuumana na Komorozine ya Comoro kati ya Februari 7 au 8, mwaka huu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic