January 10, 2014





Kipa wa Mtibwa Sugar, Said Mohamed, amesema kuwa ana mpango wa kwenda kucheza soka nchini Vietnam mara baada ya kumalizika kwa msimu huu ikiwa ni kutokana na kupata mwaliko wa kwenda nchini humo.


Said ambaye ametua klabuni hapo msimu huu baada ya kukosa namba katika kikosi cha Yanga, pia amekosa nafasi ya kuanza kikosi cha kwanza cha Mtibwa.

“Baada ya mzunguko wa pili kumalizika, natarajia kwenda nchini Vietnam kwa ajili ya majaribio, nimepata mwaliko.

“Malengo yangu kwa sasa ni kuhakikisha napata nafasi kikosi cha kwanza hapa Mtibwa ili kuwa kwenye kiwango kizuri kabla ya kwenda,” alisema Said.

SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic