January 22, 2014





Timu ya Mgambo JKT ya jijini Tanga, imeapa kukaza buti kuhakikisha inafanikiwa kutoshuka daraja msimu ujao kwa kuhakikisha inashinda michezo iliyopo mbele yao.


Mgambo ndiyo timu inayoburuza mkia kufuatia kuwa na pointi saba katika mechi 13 ilizocheza katika mzunguko wa kwanza.
Kocha Mkuu wa timu hiyo, Mohammed Kampira, alisema wamejiandaa kuhakikisha timu inafanya vizuri zaidi.

Alisema kufanya kwao vizuri ndiyo kutawasaidia kutoka mkiani mwa ligi kuu na hatimaye kubaki kwenye ligi msimu ujao.

 “Maandalizi yanakwenda vyema na tumejipanga ipasavyo kuhakikisha tunafanikiwa kushinda mechi zote za nyumbani ili kujiweka katika nafasi nzuri.
“Wachezaji wangu wote wapo katika hali nzuri ya kiushindani na majeruhi waliokuwepo hivi sasa ni wachache tu na hadi mzunguko wa pili utakapoanza watakuwa fiti tayari kwa kuanza ligi,” alisema Kampira.
Mwishoo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic