January 10, 2014





Beki wa kati wa Ashanti United, Victor Costa ameionya na kuipa mbinu Azam FC ambayo itavaana na Ferroviario da Beira ya Msumbiji katika hatua ya awali ya Kombe la Shirikisho Afrika inayotarajiwa kutimua vumbi Februari, mwaka huu.


Costa ambaye aliwahi kucheza soka la kulipwa nchini Msumbiji, amesema iwapo Azam inahitaji kusonga mbele zaidi katika michuano hiyo, inatakiwa ijipange vizuri kwa kuwa wapinzani wao hao wapo kamili.

“Ferroviario ni nzuri, nawajua hao jamaa, Azam wanatakiwa wasiidharau, hivyo siri kubwa ni kuhakikisha wanaingia wakijua wanakutana na timu ngumu la sivyo yatakuwa mengine.

“Sijui kuna mabadiliko gani ya ziada katika timu hiyo, maana ni muda mrefu tangu nilivyoondoka, lakini naamini bado wapo vizuri, cha msingi ni kujiandaa tu,” alisema Costa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic