January 20, 2014


Mshambulaiji wa JKT Ruvu, Paul Ndauka, wiki iliyopita alikutana na changamoto kubwa kwenye Mtandao wa Kijamii wa Facebook, baada ya kuandika ujumbe wa kumtetea kiungo wa Yanga, Athuman Idd ‘Chuji’.


Mshambuliaji huyo aliandika ujumbe wa kumtetea kiungo huyo na kuwataka watu waache kumfuatafuata kwa kuwa anajua alifanyalo.

Chuji kwa sasa amesimamishwa klabuni kwake kwa muda usiojulikana kutokana na utovu wa nidhamu.

Kiungo huyo aliandika: “Kila mtu Chuji kazingua, vipi jamani mbona siyo kiivyo? Acheni kumfanya Chuji kama kaua na hakuna binadamu ambaye hakosei.

“Sema wewe umekosea mara ngapi na watu wakakusamehe, makosa mengine yanaongezewa majungu na watu kama Kibadeni na flaniflani ambao hujiona magwiji wa mpira wa Bongo…”

Wengi waliochangia walionekana kuwa tofauti na Ndauka ambapo wapo waliofikia hatua ya kumtolea lugha kali na kumtaka kutoingilia maamuzi ya uongozi wa Yanga.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic