KIKOSI CHA MTIBWA SUGAR |
Beki wa Mtibwa Sugar, Salim Mbonde, juzi
Jumamosi alizimia katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam na sasa amepewa siku tatu za kupumzika.
Mbonde alizimia kwa dakika tano baada ya
kugongwa na kipa wa timu yake Hussein Sharifu ‘Casillas’ na straika wa Simba, Betram
Mwombeki wakati akiokoa mpira uliokuwa umepigwa golini kwake.
Mbonde amesema daktari wa kikosi hicho chenye maskani yake Manungu, amempa siku
tatu kwa ajili ya kumtazama kama amepona kabisa.
Alisema binafsi anajisikia vizuri na
anamshukuru Mungu kwa kuwa mzima mpaka sasa na anachukulia tukio hilo kama
sehemu ya mchezo.
“Nimepewa siku tatu za mapumziko, baada
ya hapo daktari ataniangalia tena, akiona nimekaa sawa ndiyo ataniruhusu.
“Unajua siku ile (juzi) wakati nafanyiwa
hivyo nilikuwa naokoa mpira uliokuwa umepigwa golini kwetu, sasa wakati naruka
juu nikakutana na Mwombeki na Casillas, wakanigona, baada ya hapo sikuelewa
kitu hadi niliposhtukia nipo kwenye geti la kuingilia uwanjani napelekwa
maabara,” alisema Mbonde.
0 COMMENTS:
Post a Comment