January 20, 2014

MGOSI WAKATI AKIWA SIMBA
Mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Mussa Mgosi, juzi alikuwa kivutio kikubwa baada ya kukaa benchi na mtoto wake wa kike wakati mechi ikiendelea, akiwa ni mmoja wa  wachezaji wa akiba ‘sub’.


Ilikuwa ni katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Simba uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Simba ilifungwa 1-0.

Championi lilimshuhudia mshambuliaji huyo akiwa na binti yake katika benchi ambalo wachezaji wa akiba hukaa pamoja na makocha wao.

Mgosi hakucheza kabisa mchezo huo na muda mwingi alikuwa karibu na mtoto wake huyo anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka mitatu au minne.

Hata baada ya mchezo huo, mtoto huyo aliendelea kuwa bega kwa bega na baba yake na kila kona aliyopita, alikuwa naye hata alipokuwa akifanya mahojiano na waandishi wa habari.


Akizungumza  na Championi Jumatatu, Mgosi alisema: “Binti wangu huyu alipenda siku ya leo niongozane naye na hata alipokuja uwanjani alinifuata na sikuona  kama ni tatizo.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic