January 24, 2014





Mbeya City ipo tayari kuanza mazungumzo ya awali na kipa raia wa DR Congo, Ikolonga Type, lakini zoezi hilo limeshindikana baada ya kutokuwepo nchini kwa beki kiraka wa Yanga, raia wa Rwanda, mwenye asili ya Congo, Mbuyu Twite.


Imeelezwa kuwa, Mbeya City walianza kumfuatilia kipa huyo tangu walipouona uwezo wake alipokuwa akifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Leaders uliopo Kinondoni, Dar.

Rafiki wa karibu na mchezaji huyo ameiambia SALEHJEMBE kuwa kipa huyo ameshindwa kufanya maamuzi akimsubiri Twite arudi kutoka Uturuki alikoenda kuweka kambi na Yanga kwa kuwa ndiye mwenyeji wake hapa Tanzania.

“Alimuona Type pale Leaders akamfuata akataka kuzungumza naye kuhusu usajili wa msimu ujao lakini yeye hakuwa tayari akamwambia tusubiri Twite arudi ndiyo mambo mengine yatafuata kuhusu usajili wake,” kilisema chanzo hicho.

Alipotafutwa Type alisema: “Ni kweli kuna kiongozi nimezungumza naye kuhusu Mbeya City lakini namsubiri kwanza Twite.” Mbuyu anatarajiwa kutua nchini alfajiri ya leo kutoka Uturuki.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic