January 27, 2014


Mashabiki wa soka nchini wamemuona ‘live’ kwa mara ya kwanza Kocha wa Yanga, Hans van Der Pluijm na wengi wakaonyesha kuvutiwa zaidi na kitambi chake.


Awali, mashabiki wengi wa soka walionyesha kuwa na hamu ya kumuona kocha huyo mwenye umri wa miaka 64 kama ataweza kumudu mikiki kwenye benchi.

Pluijm akawaonyesha kwamba yuko fiti na gumzo likahamia kwenye kitambi chake kwamba ‘kinavutia’.
“Aisee kocha yuko fiti, watu wana wasiwasi wa bure. Ila kitambi chake bwana, sijui kimekaaje,” alisema mmoja wa mashabiki kwenye kundi la mashabiki wa Yanga waliokuwa Uwanja wa Taifa, juzi.

“Halafu (Ernie) Brandts alikuwa hataki vitambi, lakini sasa kocha kaja na kitambi, sijui itakuwaje!” alihoji mwingine na kusababisha wengine wacheke.


Kocha aliyepita wa Yanga, Brandts alipiga marufuku vitambi katika benchi lake, vitu vingine alivyokuwa anakataa ni kutumia simu, hasa muda wa mazoezi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic