January 29, 2014




Kiungo wa Mbeya City, Kenny Ally, amepewa wiki moja kuwa nje ya uwanja baada ya kupata majeraha katika kifundo cha mguu (enka) katika mechi yao dhidi ya Kagera Sugar.
 
Mbeya City ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya timu ya Kagera Sugar juzi katika mchezo wa ufunguzi wa ligi kuu mzunguko wa pili uliochezwa katika Uwanja wa Kaitaba, Kagera.

Akizungumza na Championi  Jumatano, Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi, alisema kiungo huyo alipata majeraha katika mchezo huo wa juzi na hivyo atakaa nje wiki moja.
“Kenny Ally ni kiungo mshambuliaji wa timu yetu aliyeumia katika mchezo wa juzi dhidi ya Kagera Sugar na atakuwa nje kwa muda wa wiki moja kutokana na majeraha aliyoyapata.
“Majeruhi wengine ni kiungo Steven Mazanda ambaye anaendelea vizuri ila sijajua kama mchezo ujao atakuwepo mpaka nipate ripoti ya daktari. Francis Casto ana tatizo la kuumia enka pia ila kwa sasa anaendelea vizuri.
“Kwa upande wa mshambuliaji Mwagane Yeya, anaendelea na matibabu ya nyonga na hakufanikiwa kucheza mchezo wa juzi lakini maendeleo yake yanaridhisha,” alisema Mwambusi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic