January 20, 2014


Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi, amesema kuna ulazima ratiba ya Ligi Kuu Bara kurekebishwa kwa sababu mapumziko ya muda mrefu yanawaathiri sana wachezaji na kurudisha nyuma kiwango cha soka.


Mbeya City ilishindwa kutamba katika  michuano ya Kombe la Mapinduzi,  lakini ikikomaa kwenye mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara kwa kuwahenyesha vigogo na kushinda nafasi ya tatu, ikiwa nyuma kwa pointi moja tu dhidi ya vinara, Yanga.

Mwambusi alisema mapumziko  ya muda mrefu yanaathiri sana viwango vya wachezaji,  japo Kombe la Mapinduzi liliwasaidia kugundua matatizo yao kiufundi.

Mwambusi alisema kwa sasa anaendelea kuwaandaa wachezaji wake ili kuweza kuhakikisha wanafanya vyema katika mzunguko wa pili unaotarajiwa kuanza Jumamosi wiki hii.
“Maandalizi yanakwenda vizuri lakini mapumziko ya muda mrefu yamewaathiri sana wachezaji wangu, kama kuna uwezekano wa ratiba kubadilishwa ni bora ikawa hivyo kuliko kuchukua muda, viwango na uwezo wao unapotea lakini nashukuru hili nimeligundua mapema kupitia Mapinduzi.
“Tumebakiza siku chache sana kabla ya ligi kuanza lakini sisi matumaini yetu ni kuanza vyema na kuendelea kuutafuta ubingwa,” alisema Mwambusi.

Mbeya City itafungua pazia lake la mzunguko wa pili kwa kuvaana na Kagera Sugar ugenini kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic