January 20, 2014

KIPRE

Straika wa Azam FC, Muivory Coast, Kipre Tchetche, amesema uwepo wa Ismael Kone kwenye kikosi hicho ni ishara kubwa ya kufanya vizuri zaidi kwenye safu ya ushambuliaji wa timu hiyo katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara.


Kone ambaye pia ni raia wa Ivory Coast, ametua Azam kwenye usajili wa dirisha dogo kuimarisha safu ya ushambuliaji ya timu hiyo inayoshikilia nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.

 Tchetche alisema kuwa wanaelewana kwa kiasi kikubwa wanapokuwa uwanjani na Kone hivyo anaamini watafanya makubwa kutokana na uchezaji wao huo.

Alisema kuwa uwezo wa kiungo huyo mshambuliaji ni mzuri na ni mchezaji ambaye hahofii mabeki na huwa anajitahidi kufanya analoweza ili mradi ahakikishe anaipa ushindi timu yake, kitu ambacho kina faida kubwa kwa Azam.


“Kone ni mchezaji mzuri anayeyajua majukumu anapokuwa uwanjani, kwa hiyo mtu kama huyu unapofanya naye kazi inakuwa ni rahisi sana kufanikisha mnalolitaka kwa timu ambalo ni ushindi pekee, naamini pamoja tutafanya vizuri mzunguko wa pili,” alisema Tchetche.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic