January 31, 2014


Kocha Mkuu wa Coastal Union, Yusufu Chippo amedai kuwa msimu huu Azam FC ndiyo mabingwa wa Ligi Kuu Bara.


Chippo amesema endapo hautafanyika ujanjaujanja, Azam ndiyo itakuwa bingwa wa Tanzania Bara.

“(Coastal) Hatuna tena nafasi ya kupigania ubingwa, ila tuna nafasi ya kuhakikisha tunamaliza ligi hiyo tukiwa pazuri zaidi.

“Timu ambayo msimu huu inaweza kutwaa ubingwa huo ni Azam, nasema hivyo kwa sababu ina kila kitu ambacho kinaweza kuifanya ifikie hatua hiyo bila kuwa na tatizo lolote kuanzia uimara wa kikosi chake hadi kiuchumi,” alisema Chippo.


Azam inaongoza msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 33 ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 32 huku Mbeya City ikishika nafasi ya tatu ikiwa na 31.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic