January 31, 2014


OLABA

Kocha Mkuu wa Ruvu Shooting, Mkenya, Tom Olaba ameponda kiwango kilichoonyeshwa na timu ya Mbeya City na kudai kuwa wakiendelea kucheza hivyo hawatafika mbali.


Amesema hayo baada ya mechi ya juzi Jumatano kwenye Uwanja wa Mabatini, Kibaha baina ya timu hizo uliomalizika kwa sare ya bao 1-1.

Olaba alisema hakupendezewa na namna wapinzani wake walivyokuwa wakicheza kwa kuwa kila walipokuwa wakigusa mpira, ilikuwa ni faulo, pia wanatumia nguvu kuliko akili.


“Sikupenda namna walivyokuwa wanacheza, hawana nidhamu uwanjani, yaani asilimia 65 wanacheza faulo tu na kwa mpira huu hawatafika mbali,” alisema Olaba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic