January 17, 2014



Kocha Mbelgiji, Luc Eymael akimuomba radhi akimtaka asiamini kwamba yeye amembeza Hans van Der Pluijm.
Katika barua pepe ya kocha hiyo ambayo Championi Ijumaa limeishuhudia na kopi linayo, van Der Pluijm amemuomba radhi pia Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Abdallah Bin Kleb.


“Mimi ni kocha ninayejali taalum yangu, ninafuata weledi, hata kidogo siwezi kuzungumzia na kumponda kocha mwingine, kuna gazeti la hapo Tanzania limeandika ambacho sikusema na mwandishi amenilisha maneno.

“Tafadhari, namba niseme hivi, naomba radhi kwa kilichoripotiwa kwenye chombo hicho cha habari cha Tanzania kwamba ninasema mtafungwa na Simba milele, kitu ambacho hakiwezekani kwenye mpira,” aliandika kwenye barua pepe hiyo.

Lakini alipoulizwa na gazeti hili sababu za kuomba radhi kwa uongozi wa Yanga wakati yeye si kocha wa kikosi hicho, Eymael aliyewahi kuwa kocha wa AFC Leopards alisema:

“Uungwana ni kitu kizuri sana, nashangaa kilichoandikwa kwa kuwa si lahisi kocha mwenye akili timamu amponde mwenzake bila ya sababu. Sijawahi kuziona Yanga au Simba zikicheza, lakini Yanga si adui zangu, lazima niwaombe radhi.
“Najisikia vibaya kwa kuwa walioandika wametaka kunitegenezea maadui Tanzania bila ya sababu, nimesema vitu tofauti kabisa. Nimekasirika sana na siku yangu si nzuri tena, leo.

“Kama Yanga watanielewa, litakuwa jambo zuri kwa kuwa nimetumia uungwana. Lakini isipokuwa hivyo nitasikitika sana.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic