January 31, 2014



Mashabiki wa soka mkoani hapa wamembandika jina jipya Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm kwa kumuita Capello, wakimfananisha na kocha wa zamani wa Juventus, Fabio Capello.


Mara baada ya Pluijm kuingia uwanjani na kuanza kuwasalimu mashabiki wa timu hiyo, walimshangilia huku wengine wakimwita Capello, kocha ambaye sasa anakiongoza kikosi cha Urusi.

Baada ya kumalizika kwa mchezo huo, SALEHJEMBE iliwahoji mashabiki hao juu ya sababu za kumpa jina hilo ambapo walisema kuwa eti amefanana na Capello.


“Jamaa anafanana sana na Capello,” alisema shabiki mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Juma Hassan lakini kabla hajamaliza, mwingine aliyejitambulisha kama Ramadhan Athumani, akadakia: “Ila wanatofautiana kidogo sana kwa sababu huyu ana kitambi lakini Capello hana.” 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic