January 29, 2014


Mabao mawili ya Daniel Sturridge, moja na nahodha Steven Gerrard na moja la Luis Suarez yameisaidia Liverpool kuwavuruga watani wao wa jadi Everton kwa mabao 4-0.


Katika mechi hiyo ya watani wa jadi wa jiji la Liverpool, Everton walishindwa kuonyesha makali yao kabisa na kulala kwa mabao hayo.

Eveton ndiyo ilionekana kuwa na kikosi kigumu zaidi kufungwa katika Premiership, lakini ilishindwa kuonyesha ugumu huo na kuruhusu mabao manne.


Bahati kwa Everton ingeweza kulala kwa mabao matano, lakini Sturridge alikosa penalti kwa mkwaju aliopiga kupaa juu ya lango la watani wao hao wa jadi.

MATOKEO MENGINE:
Swansea 2 Fulham 0
Crystal Palace 1 Hull City 0
Norwch 0 Newcastle 0

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic