January 22, 2014





Katika kuhakikisha wachezaji wa Simba wanaelewa kile kinachofundishwa, kocha mkuu wa timu hiyo, Zdravko Logarusic, amekuwa akitumia neno moja la Kiswahili.


Kocha huyo ambaye ni raia wa Croatia, ameonyesha kuwa ni mwepesi wa kujifunza, kitu ambacho kimekuwa kikiwasumbua makocha wengine.

Katika mazoezi ya juzi yaliyokuwa yakifanyika kwenye Uwanja wa Kinesi jijini Dar, Loga alikuwa akikorofishana na wachezaji wake mara kwa mara kutokana na wengi wao kuonyesha kuwa hawamuelewi.

Kila mara kocha huyo ambaye amewahi kuifundisha timu ya Gor Mahia ya Kenya, alikuwa akitumia neno ‘piga’ pale alipokuwa akimtaka mshambuliaji au beki kupiga mpira.

Hata hivyo, mara kwa mara alikuwa akimuita kiungo wa timu hiyo, Amri Kiemba, ili awe mkalimani wake na kumtumia kuwaelewesha baadhi ya wachezaji kwa Kiswahili pale alipoona kuwa hawamuelewi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic