January 22, 2014





Klabu za Simba na Yanga zimeukubali uteuzi wa Juma Nkamia kuwa Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.


Nkamia ambaye aliwahi kuwa mtangazaji wa Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Kondoa Kusini kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), alitangazwa kuchukua nafasi hiyo Jumapili badala ya Amos Makalla ambaye amepelekwa kuwa Naibu Waziri Wizara ya Maji.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, viongozi wa Simba na Yanga wamesema Rais Jakaya Kikwete hakufanya makosa kumteua Nkamia katika nafasi hiyo kwani anakidhi vigezo.

“Nimefurahi kuona rais amemteua Nkamia na huenda akakumbuka alipotoka na atawaendeleza wanamichezo zaidi katika kuhakikisha sekta ya habari inakua.

“Ni nafasi yake ya kuweza kuonyesha uwezo kwani anafahamu vitu vingi vya michezo na kwa undani zaidi tofauti na wengine waliokuwa wakipewa nafasi hivyo,” alisema Beno Njovu, Katibu Mkuu wa Yanga.

Aidha, kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya Simba, Danny Manembe, alisema Simba wana imani Nkamia atasaidia soka na kuendeleza mbele tasnia ya habari kwa ujumla.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic