January 6, 2014


Timu ya JKT Oljoro inatarajia kuweka kambi visiwani Zanzibar kwa ajili ya kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kuanza Januari 25.


Oljoro kwa sasa inafundishwa na kocha mpya, Hemed Morocco, baada ya kutimuliwa kwa aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Alex Mwamgaya.

Morocco aliyeifundisha Coastal Union katika mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara kabla ya kutimuliwa, amesema anadhani Zanzibar ni sehemu nzuri kwa ajili ya maandalizi.

Morocco alisema kuwa timu hiyo itakapokuwa huko itacheza mechi mbalimbali za kirafiki ili kuweza kujiweka fiti zaidi kabla ya mzunguko wa pili kuanza mapema mwezi huu.

“Tumeamua kwenda kuweka kambi Zanzibar kwa muda mfupi uliobakia kwa ajili ya kujiimarisha zaidi kwa sababu malengo yangu ni kuhakikisha timu yangu inatoka katika nafasi iliyopo kwa sasa na kufikia nafasi za juu.

 “Tukiwa huko tutacheza mechi kama nne au tano ili kujiweka fiti, zaidi tutacheza na timu kama Mafunzo na nyingine za huko kisiwani, lengo likiwa ni kujiimarisha zaidi,” alisema Morocco.

Oljoro imemaliza mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara ikiwa katika nafasi ya 11 kwenye msimamo, baada ya kujikusanyia pointi 10, sawa na Ashanti walio katika nafasi ya 12.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic