January 7, 2014




Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amesema ana imani kubwa na safu yake ya ulinzi na anahamisha mashambulizi kwa viungo.


 Logarusic amesema katika mashindano ya Mapinduzi amefurahia safu yake ya ulinzi inavyocheza.

“Wanacheza vizuri, siwezi kusema nimeridhika, lakini naweza kusema wanacheza vizuri.
“Ndiyo maana nilitaka kumsajili Ivo na Musoti kwa ajili ya kuimarisha safu ya ulinzi.

“Ila sasa nitahamia kwa viungo kwa ajili ya kuwaweka vizuri na baadaye washambuliaji.
“Bado kuna mambo sifurahii, lakini najua, katika mafunzo lazima urudie tena na tena ili watu waelewe,” alisema Logarusic ambaye msaidizi wake ni Selemani Matola.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic