January 7, 2014





Winga nyota wa zamani wa Yanga, Edibily Lunyamila amerejea katika hali nzuri na kuwashuruku wadau.


Lunyamila amesema anajisikia vizuri tofauti na hali iliyomkuta hadi kulazimika kulazwa.
“Kweli nina nafuu kubwa, naona nimepona ingawa ninahitaji muda kurudi katika hali yangu ya kawaida,” alisema Lunyamila.

“Natoa shukurani kwa wote walionijali, walinipa faraja na walionyesha upendo wa juu kwa kweli, nashukuru sana,” alisema Lunyamila.

Winga huyo alilazwa kwa zaidi ya wiki moja kwenye Hospitali ya Mwananyamala kutokana na kusumbuliwa na magonjwa ya moyo yaliyosababisha apumue kwa tabu hadi kuwekewa mashine ya kumsaidia kupumua.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic