January 29, 2014





Kipa Yaw Berko wa Simba amekalia kuti kavu katika timu hiyo baada ya kocha mkuu wa timu hiyo, Zdravko Logarusic, kutaka amtumie Ivo Mapunda zaidi katika kikosi chake cha kwanza.


Ivo alipewa nafasi ya kukitumikia kikosi hicho katika Michuano ya Kombe la Mapinduzi iliyomalizika hivi karibuni visiwani Zanzibar na hatimaye kuibuka nafasi ya pili.

Kocha wa makipa wa Simba, Idd Pazi, alisema kuwa awali walihitaji kumpumzisha Ivo kufuatia kudaka mfululizo katika michuano hiyo, lakini kocha Loga amekataa na kutaka kumtumia kipa huyo kwa kuwa kiwango alichokionyesha kwenye michuano ya Mapinduzi ni kikubwa.

“Loga amekataa kumpumzisha Ivo kwa kuwa alihitaji kukiona kikosi chake kilichocheza Mapinduzi ndicho kicheze mechi za ligi kwani ameona ligi ni ngumu, hivyo anahitaji kumtumia ili aweze kuisaidia timu na kama ulivyoona, tumeshinda.

“Nadhani kocha tayari ameshapata kikosi ambacho ni kile kilichoshiriki Mapinduzi na iwapo kutakuwa na mabadiliko basi yatakuwa machache,” alisema Pazi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic