January 29, 2014





Uongozi wa Yanga umesema wala hauna presha na majibu yatakayotolewa na Fifa kwa kuwa tayari wameshapata ruksa kutoka Caf ya kumtumia mshambuliaji wao Emmanuel Okwi kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Komorozine ya nchini Comoro.
 
Yanga na Comorozine wanatarajia kucheza Februari 7, mwaka huu kwenye Dimba la Taifa jijini Dar ukiwa ni mchezo wa kwanza na iwapo Yanga itafuzu itakutana na El Ahly ya Misri.

Okwi alisimamishwa na Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kucheza ligi mpaka watakapopata ufafanuzi kutoka Fifa kama Yanga wanaweza kumtumia mchezaji huyo.

Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu, alisema tayari Shirikisho la Soka Afrika (Caf), limemuidhinisha na wao wanafuata kauli hiyo na siyo ya TFF kwa kuwa ligi hiyo siyo yao.

Alisema hawana hofu juu ya hilo kwa kuwa Caf ni wakubwa kuliko TFF ambao wamekataa mchezaji wao asicheze kwenye ligi yao kwa hiyo hawana hofu juu ya hilo.

“Sisi tumeruhusiwa kumtumia Okwi na Caf kwa hiyo kwenye mechi yetu dhidi ya Comorozine ataanza kuonekana akiwa uwanjani.

“Wao TFF si wamekataa tusimtumie kwenye ligi yao, sasa Caf ni wakubwa zaidi yao na tutamtumia,” alisema Beno.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic