January 29, 2014



 
MBOGO (KULIA) AKICHUANO NA MESSI WA SIMBA
Wakati mabeki wa timu nyingine za ligi kuu hapa nchini wakisuasua kuzungumzia ubora wa mshambuliaji wa Simba, Ramadhan Singano ‘Messi’, beki wa kati wa Rhino Rangers, Ladislaus Mbogo ameibuka na kusema kuwa mchezaji huyo kwa sasa ni zaidi ya Emmanuel Okwi na Mrisho Ngassa.
 
Mbogo ambaye aliwahi kuitumikia Yanga  msimu uliopita, alikumbana na kashikashi za Messi katika mchezo wa ligi kuu uliozikutanisha  timu hizo mbili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Jumapili iliyopita na Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0. 

Bao hilo pekee la Simba katika mechi hiyo lilifungwa na Messi baada ya kuwazidi ujanja Mbogo pamoja na beki mwenzake, Laban Kambole.

Mbogo amesema kuwa amewahi kupambana na Okwi pamoja na Ngassa lakini hakupata usumbufu mkubwa wa kuwakaba kama alioupata kwa Messi, Jumapili iliyopita.

 Kama nisingekuwa makini ningeumbuka, ilinibidi nitumie akili nyingi sana kumkaba,  kuna wakati ilibidi nitumie nguvu ili kumtisha apunguze kasi.

“Hivi sasa katika ligi kuu Messi ni zaidi ya Ngassa na Okwi, atakayebisha ni mwongo,” alisema Mbogo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic