January 8, 2014



Na Saleh Ally
HII ni miaka ya tabu kwa Manchester United, yaani 2013-14, hata kama kutakuwa na marekebisho, basi ndiyo kipindi kigumu sana kwa mashabiki wa klabu hiyo.

Timu yao haifanyi vizuri na inaonekana wataalamu kadhaa wanakubaliana kwa hilo wakiamini lazima kungekuwa na mtikisiko kutokana na kuondoka kwa Kocha Alex Ferguson ambaye amedumu katika kikosi hicho kwa miaka 27.

Kuondoka kwake lazima kuwe na mtikisiko, ndiyo maana kocha mpya, David Moyes amekuwa katika wakati mgumu sana akionekana ni tatizo, kinda na maneno mengi anayotupiwa, lakini uongozi umezidi kuonyesha unamuamini.


Hadi baada ya mechi 20, Manchester United ambao ndiyo mabingwa watetezi wamebaki katika nafasi ya saba wakiwa na pointi 34, tofauti ya pointi 11 na vinara Arsenal.

Marekebisho yanawezekana, ingawa taratibu matumaini ya kuwa mabingwa tena yameanza kuyeyuka taratibu, lakini kinachowatisha zaidi mashabiki wake ni hiki; hata wanapokuwa nyumbani Old Trafford bado hawana uhakika wa ushindi.


Hawana uhakika huo, kwani katika mechi 10 walizocheza nyumbani, Manchester United wamepoteza nne, sare mbili na kushinda nne tu, hii si kawaida.

Si kawaida na hasa kwenye ligi, ikitokea timu f’lani inakutana na Manchester United ndani ya Old Trafford maarufu OT basi bora kulilia sare kwa kuwa jamaa kwao ni ‘wabaya’.

Lakini sasa ni tofauti, mashabiki wake wamelalama kwamba wanaingia OT wakiwa ‘roho mkononi’, hofu ya kupata presha hata kama wanacheza na timu inayoweza kuitwa ndogo.

Mashabiki hao wanasema bora wangekuwa hawapotezi nyumbani, angalau uhakika wa pointi za OT, zingewapa ahueni lakini sasa hawajui wapi hasa Manchester United ina makali hasa.

Rekodi ya ugenini inaonyesha katika mechi 10, imeshinda 6, sare mbili na kupoteza 2. Maana yake, Manchester United ya Moyes ni bora zaidi ugenini hata kuliko nyumbani.
Hata katika ufungaji, inaonyesha katika mechi 20 za nyumbani Manchester United, imefunga mabao 12 tu na kufungwa 10, lakini ugenini imefunga 21 na kufungwa 14.
Hesabu zinaonyesha Manchester United ikiwa ugenini imefunga mabao takribani mara mbili ya yale iliyofunga nyumbani, kitu ambacho kiufundi si sahihi.
Wakati rekodi nzuri kwa timu ni kuwa bora zaidi nyumbani kwanza, halafu kuhakikisha unafanya kazi kwa uhakika kuzipata za nyumbani.
Maana yake, kama Moyes atataka kurekebisha kikosi chake kianze kupata, lazima arekebishe mwenendo wa OT. La sivyo, Manchester United itaendelea kufulia.
MABAO:
                                        NYUMBANI      UGENINI    JUMLA
Mabao iliyofunga               12                       21               33
Mabao iliyofungwa            10                      14                24

MECHI 8 ZA MWISHO:
                             P       W     D       L        Pts
Manchester City       8       7       1       0       22
Chelsea                       8       6       1       1       19
Everton                       8       5       2       1       17
Arsenal                        8       5       2       1       17
Tottenham                 8       5       2       1       17
Liverpool           8       5       0       3       15
Manchester Utd       8       4       1       3       13

MECHI ILIZOPOTEZA NYUMBANI:
Sept 28:
Man United 1 Vs West Brom 2

Des 4:
Man United 0 Vs Everton 1

Des 7:
Man United 0 Vs Newcastle 1

Jan Mosi:
Man United 0 Vs Tottenham 1

REKODI:
Mechi za nyumbani shinda 4, sare 2, poteza 4
Ugenini shinda 6, sare 2, poteza 2

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic