January 30, 2014

MWAMBUSI

Kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi amesema pamoja na kujua wamepaniwa sana kikosi chake kimepania kuendelea ushindi.

Mwambusi, amesema wanajua kila timu imepania kuvunja rekodi yao ya kutofungwa kwenye ligi, lakini wataendelea kupambana.
“Kila mmoja anataka kuwa wa kwanza kushinda dhidi ya Mbeya City, lakini na sisi tumepania kuendeleza rekodi.

“Wachezaji, benchi la ufundi na wote kwa ujumla tunalijua hilo, lakini tunaendelea kupambana,” alisema Mwambusi.

Mbeya City iliyoonekana huenda ni nguvu ya soda, ilirejea katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara kwa ushindi tena ikiilaza Kagera Sugar kwao Bukoka kwa bao 1-0.

Mechi yake ya pili, ikapambana kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya Ruvu kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic