January 29, 2014





Na Richard Bukos, Tanga
Mshambuliaji mpya wa Yanga, Emmanuel Okwi, raia wa Uganda, ambaye amesimamishwa kutokana na suala lake la uhamisho kuzua utata, jezi yake imeendelea kugombewa kama njugu na mashabiki wa timu hiyo waliokutwa na Championi Jumatano maeneo ya Uwanja wa Mkwakwani mjini hapa, jana Jumanne.

Yanga ipo mjini hapa kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Coastal Union utakaopigwa leo Jumatano.

Akizungumza na Championi Jumatano, mmoja wa wauzaji wa jezi aliyejitambulisha kwa jina la Khalid Mwalimu, alisema katika rundo la jezi anazouza, nyingi ni kama za kupamba biashara tu lakini jezi inayouzika kama njugu ni ya Okwi.

"Hizi unazoziona nimezifuata mara ya tatu, kila nikileta namaliza, nafuata nyingine, wengine wanachukua za Ngassa lakini jezi za Okwi leo ndiyo zimekuwa dili sana.

“Mpaka huko tunakochukua mzigo wa jumla nao wamesema wameshamaliza, wametuahidi labda kesho ndiyo wanaweza kutuletea nyingine," alisema Mwalimu kwa lafudhi ya kabila la Wadigo huku akiwa ameshika jezi hizo.
SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic