January 5, 2014



Mshambuliaji tegemeo wa Swansea, Wilfried Bony (pichani juu) amefunga bao la ushindi na kuiwezesha timu yake kuibwaga Man United kwa mabao 2-1 katika mchi ya Kombe la FA, leo.


Kwa kipigo hicho, Man United chini ya David Moyes imeng’olewa kwenye michuano ya FA mapema kabisa.

Bonny ndiye alimfunga kipa nyota nchini Juma Kaseja bao la nne wakati Ivory Coast iliposhinda kwa mabao 4-1 dhidi ya Taifa Stars kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, mwaka jana.

Man United pamoja na kuwa nyumbani lakini ilishindwa kufurukuta na kuambulia bao moja lililofungwa Javier Harnandez ‘Chicharito’.
Beki Fabio alilambwa kadi nyekundu na kuzidi kuongeza udhaifu kwa Man United.
Nayo Chelsea iliichapa Derby County kwa mabao 2-0 na kusonga zake mbele, wafungaji ni Mikel Obi na Oscar.

MATOKEO MENGINE YA FA LEO.
Liverpool 2 Oldham 0
Nottingham 5 West Ham 0

Sunderland 3 Carlisle 1



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic