January 10, 2014



Simba imefanikiwa kutinga fainali ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuichapa URA ya Uganda kwa mabao 2-0.

Pamoja na kutinga fainali, Simba imevunja mwisho wa kushindwa kuifunga URA kila zilipokutana na safari hii chini ya Kocha Zravko Logarusic imeonyesha mambo tofauti.

Wauaji wa URA walikuwa ni beki wao wa zamani, Joseph Owino na mkongwe Amri Kiemba ambaye ameng’ara tokea mwanzo wa michuano hiyo.
Sasa Simba itacheza fainali ya michuano hiyo Jumatatu dhidi ya KCC ya Uganda ambayo imeondoa na kuivua ubingwa Azam FC katika fainali ya kwanza leo mjini Pemba.

Katika mechi hiyo ya Simba kwenye Uwanja wa Amaan mjini Unguja, soka lilikuwa la ushindi lakini vijana wa Logarusic anayesaidiana na Selemani Matola walionyesha wako fiti zaidi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic