January 11, 2014

SIKILO 'MZARAMO', ENZI YA UHAI WAKE

Sultan Sikilo aliyefariki dunia jana saa 7 mchana amezikwa leo katika makaburi ya Kibada, Kigamboni jijini Dar.


Sikilo, mwandishi mwandamizi wa michezo na mweka hazina wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo (Taswa), alifariki dunia baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Sikilo ambaye alijulikana kwa jina la utani la Mzaramo au Mfano Mbaya kutokana na utani wa wachezaji wenzake wa kikosi cha Taswa FC atakumbukwa kwa mengi ikiwa ni pamoja na uchapakazi.

Alikuwa kati ya waandishi wa mwanzo kuliandikia gazeti la Bingwa akiwa na akina Saleh Ally, Hassan Bumbuli, Selemani Mkangara na wengine.

MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALA PEMA PEPONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic