January 10, 2014



Yanga SC wameanza mazoezi rasmi nchini Uturuki katika kambi yao ya wiki mbili.


Pamoja na hivyo, Yanga wamepata bahati ya kukutana na beki wa zamani wa Real Madrid na Brazi, Roberto Carlos.
Carlos aliyekuwa maarufu kama mashuti sasa ni Kocha Mkuu wa timu ya Sivasspor inayoshiriki Ligi Kuu ya Uturuki.


Carlos aliungana na Yanga kwenye Uwanja wa Hoteli ya Sueno Beach Side nje kidogo ya mji wa Antalya na kupiga picha na wachezaji pamoja na makocha wa timu hiyo, Charles Boniface Mkwasa na Juma Pondamali.
Baada ya hapo, Yanga waliendelea na mazoezi kujiandaa na lala salama ya Ligi Kuu Bara pamoja na michuano ya Kimataifa kwa kuwa wao ndiyo wawakilishi wa Tanzania katika Ligi ya Mabingwa Afrika.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic